Sunday, August 25, 2013

MUUZA MAZIWA APEWA KICHAPO KWA KUMZINI NG'OMBE NCHINI
Mji wa Embu.
MCHUUZI wa maziwa mwenye umri wa miaka 50 alipata majeraha mabaya, aliposhambuliwa na umati wa watu  kwa kupatikana akifanya mapenzi na ng’ombe katika kijiji cha Kabogi eneo la Kathaari, Embu Kaskazini.
Bw Nyaga Kirianye anadaiwa kufumaniwa na mkulima mmoja katika eneo hilo akimchafua ng’ombe huyo mwendo wa saa tatu na nusu asubuhi.
Mkulima huyo alipiga yowe iliyowavutia wanakijiji ambao walimpa kichapo cha mbwa kabla ya kuokolewa na naibu wa chifu wa eneo hilo.
Wenyeji walidai ya kuwa mfanyabiashara huyo ana mazoea ya kuwafukuza wake zake na inadaiwa alimfukuza mke wake wa hivi karibuni, miezi miwili iliyopita.
Bw Kirianye alijitetea kwa majirani akisema yeye huwa anavutiwa na ng’ombe huyo kwa vile hana mke.
Alipelekwa hospitalini kabla ya kufunguliwa mashtaka.

No comments: