BADO WANAUME WENGI WANANYANYASWA NA WAKE
ZAO NCHINI KENYA
WANAUME
wengi nchini Kenya wanapigwa na wake zao lakini hawaripoti visa hivyo kwa
kuogopa aibu.
Kulingana
na mshirikishi wa kitaifa wa shirika la kutetea wanaume la MenKen, Bw Fredrick
Nyaga, wanaume ndio wanaoathiriwa zaidi na dhuluma za kinyumba hata kuliko
wanawake.
“Katika
visa vyote vya dhuluma za jinsia, ni chini ya asilimia tatu pekee iliyoripotiwa
miongoni mwa wanaume ambao wamedhulumiwa na wanawake. Hii ni kutokana na wanaume
kunyamaza kwa aibu,” amesema.
Bw
Nyaga alikuwa akizungumza kwenye hafla ya kuzinduliwa kwa ripoti ya sera kuhusu
kushirikisha wanaume katika juhudi za kuzuia uambukizaji Ukimwi na dhuluma za
kijinsia katika mkahawa wa Sarova Panafric, Nairobi.
Ripoti
hiyo iliyoandaliwa na shirika la MenKen kwa ushirikiano na mashirika ya
kimataifa, inakosoa udhaifu uliopo kwenye sheria kwa sasa, ambao hauzungumzii
kwa uzito suala la kudhulumiwa kwa wanaume pamoja na watoto wa kiume.
Alitoa
wito kwa wanaume na wavulana washiriki bila kulegeza kamba katika masuala ya
afya ya jamii na kuwajibika kama wazazi.
Katika
hotuba yake, mshirikishi wa kitaifa katika mradi wa kupambana na dhuluma za
kijinsia, Bi Itumeleng Komanyane, alisema mila, tamanduni na desturi za
Kiafrika huchangia kwa kiasi kikubwa katika masuala ya jamii.
Alidai
kuwa wanaume hulaumiwa zaidi kuliko wanawake katika ndoa nyingi.

No comments:
Post a Comment